HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumatatu, 26 Mei 2014

AGONGWA NA GARI HADI KUFA

Halmashauri ya manispaa ya Iringa imeshika nafasi ya tano kitaifa baada ya kufaulisha wanafunzi waliomaliza shule za msingi kwa asilimia 82 kwa mwaka 2013.
 
Akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com ofisini kwake Afisa Taaluma wa shule za msingi mkoani hapa Bwana Salmin Mndeme alisema kuwa kwa mwaka 2013 jumla ya wanafunzi 2723 sawa na asilimia 82 walifaulu na kupata nafasi ya kuendelea na kidato cha kwanza katika shule tofauti tofauti.
 
“mwaka jana jumla ya wanafunzi 3352 walibahatika kufanya mitihani ya darasa la saba na kati ya hao wavulana walikuwa 1618 na wasichana ni 1734, na waliofanya vizuri katika mitihani yao ni wavulana 1317 na wasichana 1406 jumla wanafunzi wote waliofaulu ni 2723 sawa na asilimia 82 na kwa upande wa walioshindwa wavulana ni 286 na wasichana 314 jumla wote ni 600”. Alisema bwana Mndeme.
 
Hata hivyo alisema wanafunzi hao wote walitoka katika shule 47 zilizopo manispaa ya Iringa huku shule 41 zikiwa za Serikali na shule 6 zikiwa za binafsi na kati ya hizo shule 40 zilikuwa zinafundisha mchepuo wa Kiswahili na shule 7 zilikuwa zinafundisha katika mchepuo wa kiingereza.
 
“wanafunzi wote waliofaulu wameendelea na shule za sekondari ambapo jumla ya wanafunzi 6  yaani wasichana watatu na wavulana watatu walienda shule ya vipaji maalumu na kwa upande wa shule za ufundi walienda wavulana 6 na msichana mmoja jumla walienda saba.” Alisema.
 
Pia alizitaja shule zilizoshika tatu bora mkoani hapa ni ya kwanza ni shule ya msingi Sipto, ya pili ni shule ya msingi Umsalama na nafasi ya tatu ilishikwa na shule ya msingi Ukombozi.
 
NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni