HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumatatu, 19 Mei 2014

ULEVI NI NOMA! KIJANA AFARIKI DUNIA KWA KUNYWA POMBE KUPITA KIASI


Mwili wa marehemu Geofrey Mlelwa (26) ukiwa katika gari la polisi katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa leo 
Baba mzazi wa kijana Mlelwa mzee Guriano Mlelwa kulia mwenye kofia akitazama gari hilo la polisi lenye mwili wa kijana  wake 
Baba mzazi wa kijana Mlelwa mzee Guriano Mlelwa kulia mwenye kofia akitazama gari hilo la polisi lenye mwili wa kijana  wake 
Gari la polisi  likiwa na mwili wa kijana  huyo 


MBALI ya  jitihada  mbali mbali  zinazofanywa na makampuni ya  kutengeneza  pombe kutoa tahadhari katika  chupa za pombe  hizo  kuwa unywaji pombe  kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ila bado baadhi ya watu wameendelea  kupuuza tahadhari hizo na kuendeleza tabia ya kunywa pombe kupita kupindukia kiasi cha kusababisha kuhatarisha maisha kama  kijana mkazi wa Ipogolo mjini Iringa Geofrey Mlelwa (26) aliyeamua kukatisha maisha yake kwa unywaji pombe.

Tukio hilo la  kusikitisha  limetokea  usiku wa kuamkia leo jumatatu katika  eneo la Ipogolo mjini hapa ambapo kijana  huyo kuli katika  soko kuu wa Manispaa ya Iringa akiwa  na wenzake alipoamua kuuchapa ulabu kiasi cha kushindwa  kujitambua na kupelekea  kifo chake.


Wakizungunza na mwandishi wa habari hizi baadhi ya mashuhuda   walisema  kuwa  kijana huyo enzi za uhai wake alikuwa ni mtu wa kunywa pombe za kienyeji aina ya ulanzi na bangi ila  siku  hiyo ya tukio alionekana ni mwenye pesa  hivyo kuachana na kunywa  pombe aliyoizoea na kuanza  kunywa pombe ya kisasa kwa  kuchanganya Grant na viroba na ulanzi ndani ya chupa mmoja.

Hata  hivyo walisema sanjari na kumshauri kutumia pombe ambayo aliizoea ila  bado aliendelea kupuuza na kutumia pombe hiyo  mpya kwake kwa  kunywa  kupita kiasi.

Mbali ya  kunywa  pombe hiyo ila kijana  huyo hakuweza kula chakula chochote toka alipoanza kunywa  pombe   hiyo na alipozidiwa  rafiki yake  alimkokota na kumpeleka chumbani kwao (getho) kabla ya asubuhi kuamka na kumkuta amekufa .

Baba mzazi wa  kijana  huyo mzee Guriano Mlelwa  allithibitisha  kutokea kwa  kifo cha kijana  wake na kuwa chanzo cha  kifo hicho ni unywaji  wa  pombe kupita  kiasi .

Alisema  kuwa kwa kawaida  kijana  wake anamtambua kama ni mlevi wa pombe na mtumiaji wa madawa ya kulevya na  kuwa hata katika chumba  chake walimkutana na chupa ya pombe aina ya grant ambayo ndani yake ilikuwa imechanganywa  pombe mbali mbali pamoja na viroba (konyagi).

Hivyo alisema anaamini kuwa mchanganyiko  huo wa pombe na matumizi ya dawa  za kulevya ndio umesababisha  kifo hicho hivyo  kuwashauri  vijana  kuachana na matumizi ya pombe kupita kiasi na madawa ya kulevya kwani  wakiendelea  kilichomuua mwenzao ndicho kitakachowaua pia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni