HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumatatu, 26 Mei 2014

MWENYEKITI CCM WILAYA YA NJOMBE AFARIKI GHAFLA.

late_65549.jpg
Aliekuwa mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Njombe, Adam Ismail Msigwa (pichani) ambaye alijukana kwa jina maarufu kama 'Shilingi ni Vita' amefariki jana usiku wa kuamkia leo nyumbani katika Mitaa wa Kwivaha Njombe mjini na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho kijijini kwake Lusitu.
Marehemu Adam Msigwa ambaye ni baba mlezi wa mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Iringa, Jesca Msavatavangu ambaye ni mjombe wake na Spika wa Bunge, Anna Makinda amefarika dunia jana usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua ghafla kwa ugonjwa wa shinikizo la damu (BP) pamoja na matatizo ya moyo. (NA FRIDAY SIMBAYA, NJOMBE)
msiba_e3922.jpg
Mwenyekiti wa Wilaya ya Njombe mjini, Adam Msigwa (mwenye kofia) enzi za uhai wake akiwa na Mkuu wa Wilaya Njombe Sarah Dumba wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2011.
mramba_c071f.jpg
Marehemu Adam Msigwa (kulia) akiwa na Bazili Mramba enzi za uhai wake.
mkuu_16922.jpg
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Capt. Aseri Msangi (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na mdogo wa marehem, Abubakari Msigwa (wa mwisho kulia) walipofika nyumbani kwa marehemu leo asubuhi.
mkapa_f85d4.jpg
Marehemu Adam Isimail Msigwa (kulia) akisalimia na Rais mstaafu Benjamin William Mkapa mwaka 1995 enzi za uhai wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni