HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Ijumaa, 6 Juni 2014

MBUNGE MGIMWA AANZA KUTIMIZA AHADI ZA MAREHEMU BABAKE KWA KASI KUBWA


'Hongera  sana mheshimiwa kweli umeanza kwa mfano "
Katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Iringa Denis Lupala kulia akimpongeza diwani wa kata ya Nzihi kwa kazi nzuri 
Wananchi wa Ilala  Simba  wakimsikiliza mbunge Mgimwa 
Uongozi wa kijiji cha Ilala Simba  ukimkabidhi mbunge Mgimwa risala yao 
Mbunge Mgimwa akikabidhi mipira  kijiji cha Ilala  Simba leo 
Sehemu ya  saruji  iliyotolewa  leo na mbunge Mgimwa 
Mbunge  wa  jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Nyamihuu katika  ziara  yake ya  kuwashukuru na kupokea  changamoto mbali mbali 
Mmoja kati ya  wazee  walemavu kijiji  cha Nyamihuu kalenga  akimwomba mbunge Mgimwa msaada wa baiskeli ya  walemavu 
Kiongozi wa  serikali ya  kijiji cha Nyamihuu akipokea mipira kwa ajili ya kuendeleza michezo kwa  vijana
Wazee kijiji cha Nyamihuu wakimpa baraka na kumpongeza mbunge  Mgimwa  kwa uchapa kazi wake 
Bw  Kiswaga  akimpongeza mbunge Mgimwa kwa kuonyesha usikivu mkubwa kwa wananchi 
Wananchi wa kijiji cha Nyamihuu wakimshangilia mbunge Mgimwa  leo 
Wananchi wa Kidamali  wakimsalimia mbunge Mgimwa leo  huku  wakifurahia utendaji kazi wake 
Mbunge Mgimwa akifurahi na  watoto wa kijiji cha Kidamali  waliofika  kumsalimia 
Mbunge Mgimwa akisalimiana na  wananchi pamoja na watoto  waliomng'ang'ania leo amini ni mbunge  wa  wote 
Diwani wa kata ya Nzihi Stivin Mhapa akimpongeza mbunge Mgimwa  leo 
Wananchi wa Kidamali  wakimsikiliza mbunge Mgimwa kwa umakini mkubwa 
Katibu mwenezi wa CCM Iringa Danis Lupala akimkaribisha mbunge Mgimwa  leo 
Mbunge Mgimwa akiwashukuru  wakazi wa Kidamali 
Mbunge Mgimwa  kulia akikabidhi mipira kwa vijana leo 
Mbunge Mgimwa  kulia akikabidhi msaada wa  saruji mifuko 50 kwa ajili ya kuchangia ujenzi kijiji cha Kidamali leo 
Mbunge Msigwa akikabidhi fedha  taslimu kiasi cha Tsh 500,000 kuchangia  michezo na ujenzi wa  soko 
Mbunge Mgimwa akisalimiana na  wananchi wa kidamali  leo 

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Magubike Bi Lenatha Mbilinyi kushoto akipokea msaada wa saruji mifuko 100 kutoka kwa mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa leo ,wanaoshuhudia  kulia ni katibu menezi wa CCM wilaya Denis Lupala na diwani wa kata ya Nzihi katikati Bw Stivin Mhapa
........................................................................................

MBUNGE  wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa  Godfrey Mgimwa ameanza  kutimiza ahadi  zake kwa  wananchi  wa  jimbo la kalenga  kwa  kukabidhi mifuko zaidi ya 150 ya  saruji katika  kijiji cha Magubike na kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi  yenye  thamani  ya zaidi ya Tsh milioni 2.5


Saruji  hiyo mifuko 100 kwa ajili ya  kusaidia ujenzi wa jengo la utawala shule ya  sekondari Dimitrios katika  kijiji  cha Magubike  na mifuko 50 kwa ajili ya shule ya sekondari Kidamali.


Mgimwa alisema kuwa lengo la kutimiza ahadi  yake  hiyo ni kama njia ya  kuwashukuru  wana Kalenga kwa kumchagua katika uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni pia kutimiza ahadi mbali mbali binafsi ambazo alizitoa mbunge aliyefariki marehemu Dr Wiliam Mgimwa.


Alisema ataendelea  kutimiza ahadi  binafsi zilizotolewa na marehemu Dr Mgimwa kulingana na uwezo  wake  na zile  za  kitaifa ambazo zipo katika Ilani ya CCM atahakikisha anaikumbusha  serikali  ya CCM ili  kutimiza ahadi hizo kwa  wakati.

“Ndugu  zangu wananchi  mbali  ya  kuwa  ubunge  wangu ni  wa  mwaka mmoja  ila  tayari  mimeanza  kutimiza ahadi  bila  ya kuchelewa  na  ninawahakikishieni  sita  waangusha  nitaendelea  kufanya  hivyo  zaidi  mniombee  uzima”


Alitaja  maeneo  ambayo tayari  amekabidhi  ahadi  zilizotolewa na mbunge aliyefariki  kuwa ni pamoja  na Kiwere shule ya msingi mifuko 80 ya saruji,shule  ya msingi wangama bati 100 na  saruji mifuko 50,shule ya msingi Negabii bati 100 ,shule ya msingi Mibikimitali bati 50 ,Kijiji cha Isupilo bati  50 na saruji mifuko 50 na maeneo mingine mengi.


Pia amekabidhi kiasi cha  Tsh 500,000 kwa ajili ya kuchangia kuwezesha  kusajili  timu ya  kata ya Nzihi na nyingine  kwa ajili ya ukarabati wa soko

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni