HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumanne, 20 Mei 2014

CHAWATA IRINGA WAPINGA UJENZI WA DARAJA

 Chama Cha Walemavu mkoani Iringa CHAWATA  kimeonekana kupiga hatua baada ya kujenga daraja la kuelekea katika ofisi zao.
 
Akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com ofisini kwake Katibu wa Chama Cha Walemavu Mkoani Iringa Bwana Haruna Mbata alisema kuwa toka wameingia madarakani mwezi wa kwanza mwaka huu walikuwa na mipango mingi sana mmoja wapo ni huo wa kujenga daraja la kuingilia ofisini kwao ambapo wameweza kulitimiza lengo hilo.
 
“tulikuwa na mikakati mingi mmoja wapo ulikuwa ni huu wa kutengeneza hilo daraja hapo nje maana watu wanashindwa kupita hapo hasa watu wenye ulemavu wanapokuja kujadili mambo ya vikoba vyao na ndipo tukaamua tulijenge haraka hili daraja hivyo tukafanya harambee ambapo mgeni rasmi alikuwa Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi ambapo tulichangisha michango na tukapata ela ya kujengea hili daraja.” Alisema Mbata.
 
Hata hivyo alisema baada ya kukamilisha daraja kwa sasa wana mpango wa kutengeza choo kwa ajili ya matumizi ya watu walio na ulemavu ambapo wakimaliza choo watajenga ofisi ambayo itakuwa ikitumika na wao wenyewe na kusema wanataka wabadilishe mazingira ya ofisi yao yaweze kutumika na kila mtu hususani kwa watu walemavu.
 
“kuna ofisi nyingine unakuta mtu mlemavu hawezi kuingia ndani anaishia nje tu ofisi inakuwa ina ngazi nyingi kitu ambacho kinampelekea kushindwa kufanikisha kilichompeleka sasa hapa tunataka tuweke mazingira ambayo yatamfanya mtu wa aina yeyote ile aweze kuingia na kufanikisha kile kilichomleta.” Alisema
 
Pia amewashukuru wananchi kwa kushirikiana nao mpaka wamefanikisha kujenga daraja hata hivyo alitoa wito kwa serikali na wananchi kwa ujumla kuona kuwa kuna mahitaji muhimu kwa walemavu na kushirikiana nao ili kuweza kujenga Taifa la kesho.
NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni