Na matukiodaimaBlogu.  
WAKATI
 maadhimisho ya  siku ya mlipakodi nchini yameadhimisha leo nchini kote 
mamlaka ya mapato  Tanzania (TRA) mkoa  wa Iringa  imekabidhi  tuzo  
mbili kwa a makampuni mawili  yanayomilikiwa na familia ya kamanda wa UV
 CCM mkoa  wa Iringa Bw Salim Asas likiwemo kampuni la  usafirishaji  
mizigo   la Asas Transporters Co. Ltd     na  ile ya   usafilishaji wa 
mafuta ya  TransFuel Logistics Ltd  baada ya  kuongoza  kwa  ulipaji 
mzuri  wa  kodi kwa mwaka 2013 /2014. 
 
 
Akitangaza 
 washindi hao   wakati  wa maadhimisho ya  siku ya mlipa kodi 
yaliyofanyika  kimkoa katika ukumbi wa IDYDC  mjini Iringa meneja  wa  
mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa  wa Iringa 
 Rosalia Mwenda alisema  kuwa    TRA  imekuwa na utaratibu  wa  
kuadhimisha  siku ya mlipa kodi nchini na kuwa kwa  mkoa wa Iringa na  
Njombe maadhimisho hayo yamefanyika katika mkoa  wa Iringa  kutokana na 
mamlaka  hiyo  kuendelea kufanya kazi kama mkoa mmoja . 
  
Alisema 
 kuwa kampuni  hizo  za  Asas  zimeweza  kuongoza katika  ulipaji kodi 
katika kipengele  cha mfanyabiashara mlipaji kodi mkubwa baada ya  
makampuni mawili  yanayosimamiwa na Asas moja kushika nafasi ya kwanza 
ambalo ni  lile  kampuni ya  usafirishaji ya Asas Transporters  C. 
Ltd    kwa  ulipaji kodi  na nafasi ya  pili ya walipaji kodi wa kati  
pia imechukuliwa na  kampuni ya usafirishaji  mafuta ya Transfuel 
Logistics Ltd ambayo  pia  ni  sehemu ya makampuni ya shiriki ya Asas  
  
Aliwataja 
 wengine   walioongoza katika  ulipaji kodi  kuwa ni pamoja na MT Huel 
Transporters , ambayo  ilishika nafasi ya  pili na nafasi ya tatu  kwa  
walipaji  kodi wakubwa ni  pamoja na Ruaha  University  College   huku  
upande  wa  walipaji  kodi  wa kati  aliyeongoza na Iringa Foods and  
Deverages Ltd  nafasi ya  pili Transfuel Logistics Ltd na nafasi ya tatu  Kalenga West Parki Tours MOtel Ltd . 
  
Wakati kwa  wafanyabiashara  wadogo  
walioshinda  tuzo  hizo  za  vyeti  maalum  nafasi ya  ya kwanza  
alipewa BEder F. Kileo nafasi ya  pili  ilichukuliwa na Shakra  Kiwanga 
 ambae ni mwenyekiti  wa UWT  wilaya ya  Iringa na nafasi ya  tatu  
ilichukuliwa na Ahmed Tasha wakati  kwa  mshindi  wa  jumla  kwa mkoa wa
 Iringa na kanda ya nyanda  za  juu  kusini akipewa  tuzo hiyo Sao Hill 
Forest Project . 
  
Kwa 
 upande  wa  vituo vya  radio   kampuni ya  Big  Time  Hinghland  
co.Ltd(Radio  Ebony Fm) nafasi ya  pili kampuni ya  Scope Tanzania Ltd (
 Radio Countyr  Fm) na nafasi  ya  tatu Qiblatain  Fm  Radio . 
  
Wakati 
 kwa upande  wa  walipakodi  bora  wilayani  kwa    Mufindi ni SAo Hill 
Forest Project  iliyoshika nafasi ya  kwanza na ya pili na ya tatu  
kuchukuliwa na Chai Bora Ltd  wakati  wilaya ya Ludewa  ni John  Naoel 
Haule   ,nafasi ya pili  ni Donata Linus MGaya  huku nafasi ya tatu   ni
 Nathanael Mgaya ,  katika  wilaya ya  Makete  aliyeongoza ni Felix 
Eliud Sanga , Christopher s.   Mahenge  na  nafasi ya Tatu ni 
Shaibustolen  Mahenge . 
  
Wilaya
 ya  Njombe  mshindi  wa kwanza ni  Philemon N . Mtewele   nafasi ya  
pili ni Augustino L . Kisinga  na nafasi ya tatu kwa  ulipaji kodi ni  
Ndimi Enterprises Ltd . 
  
Akizungumza  baada ya  kukabidhiwa   tuzo  hiyo  mkurugenzi  wa kampuni  za  Asas  
Bw  Salim Abri asas  ambae ni kamanda wa UV CCM mkoa  wa Iringa  alisem a
 kuwa  wajibu  wa kampuni yake ni  kuendelea  kulipa kodi vizuri kama  
sehemu ya  kukuza uchumi wa Taifa na  kuwa  tuzo hizo ni  heshima kwa 
kampuni  zake na kuwa  ni chachu kwa  wengine  kupenda  kulipa kodi . 
 
  
Pia 
 alisema  wapo ambao wanafikra  tofauti  kuwa  ukiwa mwanasiasa  ni mtu 
 wa  kukwepa  kodi na  kuwa kampuni  zake  zipo kwa ajili ya  kuona  
uchumi wa Taifa  unakua  pamoja na kulipa  kodi kwa  wakati na  kwa 
mujibu  wa taratibu za  nchi . 
 
Hata 
 hivyo  alisema kuwa ukwepaji  kodi  hausaidii hata  kidogo kwa ukuzaji 
wa uchumi wa Taifa na  kuwa kila mfanyabiashara  anapaswa  kuwa mzalendo
 na Taifa  lake kwa  kulipa  kodi badala ya  kukwepa  kulipa  kodi . 
 
"
 Na mimi napenda  kushukuru  sana TRA kwa utaratibu  huu wa  kuwatambua 
walipaji kodi wazuri na kuwapa vyeti hii ni heshima  na changamoto  
kubwa kwa wafanyabiashara  wengine  kulipa  kodi vizuri " 
 | 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni