HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumamosi, 22 Novemba 2014

KAMPUNI YA CONTINENTAL RELIABL CLEANRING (T) LTD YAJIVUNIA KWA UAMINIFU WA ULIPAJI KODI NCHINI

Hiki  ndicho  cheti  cha ushindi ambacho kampuni ya Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd  inayounda  pia kampuni  za  Fm Abri na Famari Inverstment (T) Ltd
Wawakilishi  wa kampuni ya Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd and Fm Abri /Famari Inverstment (T) Ltd wakiwa katika maadhimisho hayo ya TRA mkoa  wa Dar es Salaam jana
Mwakilishi  wa Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd and Fm Abri Bw  Fahad Abri  akiwa katika ukumbi  huo
Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd  wakiwa katika ukumbi huo

KAMPUNI ya kizalendo ya  Continental Reliable Cleanring (T)   Ltd iliyopo  chini ya kamapuni ya  Fm Abri na Famari Inverstment (T) Ltd  yenye makao  yake mjini Iringa na Dar es  Salaam  imejipongeza  kwa  kufanikiwa  kuongoza nafasi ya  tatu katika mkoa  wa Dar e Salaam  kwa  ulipaji mzuri  wa  kodi nchini.

Akizungumza  mara  baada ya  kukabidhiwa   cheti hicho jana katika  maadhimisho ya  siku ya mlipa  kodi yaliyofanyika kitaifa  katika Ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere,Jijini Dar es Salaam  mkurugenzi mtendaji  wa kampuni hiyo Bw Abbdalallah Abri  alisema  kuwa kampuni  yake  inajivunia kwa  kushika  nafasi ya  tatu kwa mkoa  wa Dar es Salaam  kwa  ulipaji mzuri wa  kodi.

Hapa  hivyo  alisema mafanikio hayo  yanaiwezesha kampuni  hiyo  kuendelea  kujenga  heshima  kubwa katika Taifa ila  pia  kuongeza  ufanisi  zaidi  wa utendaji kazi  wake na hali ya uaminifu ambayo  ndio msingi mkubwa kwa maendeleo ya Taifa .

Abri  alisema  kuwa  ili  Taifa   kuendelea  kujenga uchimi imara   ni  wajibu  wa kila mfanyabiashara   kuonyesha  uzalendo wake  kwa  kulipa  kodi na kuwa   wao kama wamiliki  wa kampuni ya  kizalendo ya Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd iliyopo chini ya kamapuni ya  Fm Abri  na Famari Inverstment (T) Ltd kamwe  hawatakuwa  nyuma katika ulipaji  kodi  nchini.

" Kweli  tunajivunia nafasi hii ambayo tumeishika kuwa nafasi ya tatu kwa  mkoa kama Dar es Salaam ambao  una makampuni  mengi zaidi na  wafanyabiashara wengi  wakubwa ni jambo la  kujivunia sana "

Hata  hivyo  alisema  kuwa  ushindi  ambao kampuni hiyo  imeupata  wa  ulipaji kodi  ni heshima  pia  kwa  wateja  wake ambao  wameendelea  kujenga imani na kampuni  hiyo kwa kuendelea  kuitumia katika uagizaji  mizigo mbali mbali yakiwemo magari na  kuwa heshima hiyo itaendelea  kujengwa  zaidi na makampuni   yote yaliyopo chini ya Continental Reliable Cleanring (T)  Ltd  na mengine  yanayomilikiwa na Fm Abri .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni