Jeshi
 la Magereza litafanya Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini tarehe 20 
Juni, 2014 kuanzia saa 2:00 asubuhi katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa 
wa Magereza Ukonga, Dar es Salaam ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(MB).
 Kwa mujibu wa taarifa rasmi 
iliyotolewa leo Juni 18, 2014 na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza,
 John Casmir Minja Maadhimisho haya ni ya pili kufanyika tangu Jeshi la 
Magereza Tanzania lianzishwe rasmi mwaka 1931. Madhumuni ya Siku ya 
Magereza ni:-
   a) Kuelimisha jamii juu ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza katika
       utekelezaji wa majukumu yake ya uhifadhi na Urekebishaji wa wahalifu kupitia shughuli za
       viwanda Vidogo Vidogo, Ujenzi, Kilimo, Ufugaji na Ufundi katika fani mbalimbali.
   b) Kuelimisha na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika suala zima la
       Urekebishaji wa wahalifu na;
   c) Kutoa elimu kwa umma juu ya huduma na taratibu za Uendeshaji wa Magereza Nchini.
 Shughuli zitakazofanyika siku 
hiyo ni pamoja na ufunguzi wa Duka la Bidhaa zisizolipiwa Kodi (Duty 
Free Shop) Gereza Keko, kukagua shughuli zinazofanyika kwenye Ofisi za 
Chama cha Ushirika wa Kuweka na Kukopa kwa Watumishi wa Jeshi la 
Magereza (TPS SACCOS) eneo la Keko, kufungua Karakana ya Uhunzi Gereza 
Ukonga, Gwaride Maalum, Onesho kutoka Kikosi Maalum la utayari wa 
Kutuliza Ghasia Magerezani. Ushuhuda wa Mfungwa  aliyepata Shahada ya 
Sheria (LLB) akiwa gerezani, Burudani Maalum ya muziki kutoka kwa 
wafungwa, askari wa kike waliohitimu mafunzo maalum kukabidhiwa vyeti na
 Mgeni rasmi na maonesho ya kazi mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la 
Magereza.
 Vyombo vya Habari na Wananchi 
wote wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa jirani wanakaribishwa kuja 
kushiriki katika Maadhimisho haya ili wapate nafasi ya kuona na 
kujifunzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza.
 Imetolewa na;
Lucas Ambrose Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
Afisa Habari Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
18 Juni, 2014,
DAR ES SALAAM.
Lucas Ambrose Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
Afisa Habari Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
18 Juni, 2014,
DAR ES SALAAM.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni