Rai hiyo imetolewa jana na Katibu mkuu wa mkoa wa vyuo vikuu 
vya Chama cha mapinduzi, Christopher Ngubiagai, alipokuwa  akitunuku 
vyeti kwa viongozi waliomaliza muda wao miaka mitatu kutoka vyuo vikuu 
vya Arusha na Tumaini (Makumira) kwenye mahafali ya wanachuo hao wa 
mwaka wa tatu hafla iliyofanyika chuo kikuu cha Arusha.
Aliwaambia wahitimu hao wa mwaka
 wa tatu katika vyuo hivyo kuwa wasiridhike na kiwango cha elimu 
waliyoipata bali waongeze bidii kwa kuwa vyuoni ni mwanzo tu wakupata 
mafanikio katika maisha.wajiendeleze zaidi ili kuhimili soko la 
ushindani la kielimu katika nchi za Afrika mashariki na mataifa mengine 
Ulimwenguni.
Ngubiagai, ambae pia ni mjumbe 
wa halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi,(NEC) alisema kuwa  kipindi 
kilichopo sasa ni kwa wasomi hao kutambua kuwa ajira kwa sasa hazipo na 
zinazopatikana hazitoshelezi mahitaji hivyo  ni lazima wajiandalie 
mazingira ya kujiajiri na si vinginevyo.
Alisema ni bora wasomi 
wakalitambua hilo mapema wataweza kuondokana na mawazo na fikra za 
kuajiriwa ambazo hazipo bali fursa iliyopo ni kujiajiri na wasisome kwa 
matarajio ya kuajiriwa ndani ya serekali au sekta binafsi.
‘’Ndugu zangu ninataka niwaeleze
 ukweli kwamba ajira zinazopatikana hazitoshelezi hivyo kikubwa ni ninyi
 wasomi wa vyuo vikuu  kusoma Kwa kujijengea mazingira ya kujiajiri na 
mafanikio yatapatikama.’’alisema ngubiagai.
 Na kamwe  wala wasitarajie 
kupata ajira kwa urahisi kutokana na ongezeko la wasomi wanaohitimu vyuo
 vikuu kila mwaka hapa nchini.
Aliwaambia wanavyuo hao kuwa 
Chama cha mapinduzi kimerejesha matawi  ya Chama kwenye vyuo vikuu ili 
kufundisha, itikadi ,malengo, ilani, Katiba ya CCM,elimu ya kujitegemea 
na uzalendo .
Ngubiagai, aliwaambia wasomi hao
 kuwa Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi katika kurejesha matawi hayo  
imepitisha kanuni  ambapo kutakuwa na katibu mtendaji wa  mkoa wa vyuo 
vikuu,wajumbe4 watano wa NEC, na wasomi watatu ,ambao wote watakuwa ni 
wajumbe wa NEC.
Kuhusu mikopo inayotolewa na 
bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, Ngubiagai, amewaambia kuwa 
haitoshelezi kutokana na ongezeko la vyuo vikuu nchini hivyo wasomi 
hawana budi kukaa pamoja na kutafuta ufumbuzi ili mikopo iweze 
kutosheleza mahitaji.
Akifafanua tuhuma zinazotolewa 
na vyama vya kisiasa kuhusu ziara ya Katibu mkuu wa CCM, Komredi, 
Abdulahaman Kinana, kuandamana na mawqaziri , watendaji wa serikali na 
halmashauri kwenye ziara zinazofanywa na katibu mkuu huyo.
Ngubiagai, alisema kuwa Kinana 
ndie katibu mkuu wa CCM, anakagua uhai wa Chama na utekelezaji wa Ilani 
ya uchaguzi iliyoiweka na serikali ya CCM, madarakani, Ilani ambao ni 
mkataba kati ya wananchi na serikali yao.
Pia ziara hiyo inapokea na 
kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi ndio maana Katibu mkuu
 huyo anaambatana na mawaziri, au watendaji wa serikali na halmashauri 
ili kufafanua kero na kutoa majawabu sahihi .
Awali mwenyekiti wa tawi la chuo
 kikuu cha Arusha, Daniel Limbu, alisema kuwa  tawi hilo lilianza mwaka 
2007 likiwa na wanachama 50 ,kutokana na chamgamoto zilizxojitokeza 
kipindi kilichopita, hivi sasa tawi lina wanachama zaidi ya 250 amao 
wote ni wanavyuo vikuu vya Arusha na  Tumaini.
Alisema kuwa katika mahafali hayo  wanachama 80 kutoka katika vyuo hivyo wamehitimu masomo yao vyuoni hapo,
Aliongeza kuwa vyuo hivyo pia vimepokea wanachama wapya zaidi ya 50 ambao ni wanavyuo mbali mbali hapa mkoan

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni