HOPE SERVICE STATION

nsekwa

ALTEZA

Jumamosi, 31 Mei 2014

FAMILIA YA JAMES MWAISUMBE IRINGA NA MBEYA ,INAMKUMBUKA MAMA YAO MPENDWA GRINA JAMES MWAISUMBE NI MWAKA MMOJA SASA

Familia ya James Mwaisumbe ya Iringa na Mbeya inapenda  kuwashukuru  wote  walioshiriki mazishi ya mama yao mpendwa na pia  wale  wote  wanaoendelea  kuelekeza maombi yao kwa famili  hii.

Ikumbukwe ni Tarehe 1/6/2013 ndipo mpendwa  wetu Grina James Mwaisumbe alipotutoka hapa duniani na  sasa  kesho  jumapili anafunga mwaka mmoja toka alipotutoka ,hivyo familia inaendelea kumwombea na kumkumbuka  kutokana  na ucheshi wake na ukarim na upendo mkubwa alioonyesha enzi  za uwepo  wake hapa duniani.

Grina anaendelea  kukumbukwa na mume  wake mpendwa mchungaji James Mwaisumbe ,watoto Frank ,Mpeli ,Tukuswiga,Neema, Anna na  wajukuu zako wote pamoja na ukoo wote wa akina Mwaisumbe na Msika popote  walipo.

Tunaendelea  kuamini  kuwa tulikupenda  sana na ulitupenda  zaidi ila Mungu muweza wa  yote amekupenda  zaidi yetu  hivyo hatuna budi kuendelea kukuombea kwa Mungu .

Zaidi tutaendelea kuenzi yale  yote  uliyoonyesha  enzi za uhai  wake  ikiwa ni pamoja na kuishi vema na  watu .

Bwana alitoa na Bwana ametwaha  jina lake na lihimidiwe  milele  Yote
Amina

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni